Tuesday, September 13, 2011

MAAFA: RUSHWA ya Rambirambi!

Ndugu wananchi wenzangu, nawapa pole tena kwa msiba na majanga yanayoendelea kujitokeza katika nchi yetu!
Meli iliyotengenezwa mwaka 1967 yenye uwezo wa Kubeba watu 600 ilizama
ikiwa na watu zaidi ya 1,000 ndani! KWA TANZANIA kubaini kwamba
hapa kuna makosa au Uzembe inahitaji tume.
Juzi wakati ajali ya Zanzibar ikitokea, kuna ajali nyingine ya namna kama hiyo hiyo iliyotokea Uchina. Kule China walikufa watu 12 wakati Zanzibar haijajulikana ni wangapi - wengine wanasema ni 250, wengine mia 300 wengine 600!
Katika hali ya kawaida, vyombo vya uokoaji kama hiki kilipaswa kutumiwa
na watu wachache zaidi, kusingekuwa na uzembe wa kuzidisha abiria kwenye Meli.


Mara baada tu ya ajali ile ya China, Serikali ya China ILIWAFUKUZA KAZI MAAFISA WATATU wa nafasi tofauti tofauti hata kabla ya uchunguzi haujaanza! Nilipofuatilia kwa nini walifukuzwa nikapata kufahamu kwamba ilibainika kuwa Chanzo cha Ajali ni kuzidishwa kwa Abiria na Mizigo katika ule Mtumbwi. 


Kuzidishwa kwa Abiria na Mizigo kwenye Mtumbi, kwa Wachina, halikuhitaji kuafanya uchunguzi ili kujua kwamba kuna uzembe umefanyika, na haihitaji uchunguzi kuelewa ni nani aliyezidisha Abiria! WAKAFUKUZWA KAZI MARA MOJA!!!


Hapa Tanzania, kumekuwa na mifululizo ya majanga na maafa ambayo mengi kati ya hayo yameonesha wazi kuwa kuna makosa au uzembe ambao umekuwa ukifanywa na watu/watendaji. Reaction ya Watanzania - kwa maana ya serikali mara nyingi huwa ni kutanguliza "Salaam za Rambirambi", Pole Nyingi, Pesa za Kugharimikia Mazishi, Fedha za Rambirambi, Kutembelea Wafiwa, Viongozi Kuhudhuria Mazishi n.k.


Kwa upande wa uwajibikaji hatima huwa ni ahadi ya kuundwa kwa Tume za Uchunguzi ambazo mara nyingi hata taarifa zake huwa ni Siri!!! Hausikii watu wakiwajibishwa achilia mbali wazembe kujiwajibisha wenyewe kwa kuachia ngazi!


MGOMO WA MAOMBOLEZO
Zamu hii mimi Binafsi nimeamua kwamba SIOMBOLEZI TENA - NATAKA HATUA ZICHUKULIWE! Hakuna sababu ya kuendelea kuisifu Serikali na kuiunga mkono katika ugawaji wa fedha kwa ajili ya Rambirambi na Mazishi ya Ndugu zetu wakati hakuna mtu anayehitaji rambirambi - WATU TUNATAKA UHAI WETU!


RUSHWA YA RAMBIRAMBI
Utaratibu wa Utoaji wa Rambirambi kutoka serikalini unatia mashaka zaidi. Wwakati watu wakiwa na majonzi, kuwapelekea pesa na viongozi kuwatembelea ni jambo jema, lakini linaweza kuwa na madhara makubwa mbeleni - na limeshakuwa hivyo.
Kuwahi kwa viongozi katika matukio kama haya huwa ni kwa muhimu, lakini
inakuwa tatizo sana pale kunapotumika kama "Rushwa" ya kuwapoza
 wananchi wasidai uwajibikaji kutoka kwa Viongozi hao.
Yanapotokea majanga, mara zote wananchi wameshakuwa na mtazamo wa kusubiria rambirambi za Serikali. Wakati ni jambo jema kuwafariji watu wanapokuwa wamepatikana na maafa, kitendo hiki hakipaswi kabisa kuchukuliwa kama njia ya kuwanyamazisha wananchi wasihoji na kutaka uwajibikaji kutoka Serikalini.


Mifano ya MV Bukoba, Mabomu, Spice Islanders.. n.k.
Maafa makubwa yaliyotokana na Ajali ya MV Bukoba, Mabomu ya Mbagala na Gongo la Mboto na hii ya juzi ya Zanzibar zinazidi kuamsha ari yangu ya kutaka kuelewa Suala la UWAJIBIKAJI linasimama wapi? Nadhani ni wakati muafaka wananchi tuamue kuanza kudai na kuweka uwajibikaji kwanza kwenye majanga yanayoambatana na Uzembe na Mazoea ya Kutokuwajibishwa!
Milipuko wa mabomu ya Gongo la Mboto na Mbagala Dar es Salaam ilisababisha
maafa na hasara ya mali, Serikali ilitoa pesa nyingi kwa ajili ya Rambirambi, Mazishi,
kugharimikia Makazi n.k. Lakini Uwajibishwaji kwa Wazembe haujaonekana kwa wananchi!


Ni wakati Watanzania Tuanze kuongea Uwajibikaji badala ya Kuendelea Kujifariji na Rambirambi. Sikatai Rambirambi, lakini naerejea kusema, isitumike kama Rushwa ya Kuwanyamazisha Wafiwa na Wanachi kwa ujumla wasidai Uwajibkaji ndani ya Watendaji.


..wasaalam

Wednesday, September 7, 2011

KIKWETE: Unauza Almasi kwa Pipi?

Hivi karibuni Mtandao 'tata' duniani wa WikiLeaks umeibua mengine mapya, na kama kawaida, Tanzania haikukosekana katika hizo nyaraka.


Kumuhusu KIKWETE, ni taarifa kwamba alipewa "rushwa" na mmilikuwa wa Hoteli ya Kempiski - mwarabu Ali Albwardy. Kwa uelewa na uzoefu wa Viongozi wa Kiafrika, sikushangaa wala sikuona ajabu kwamba kitu kama hicho kinaweza kutokea....


Kiongozi wa kiafrika kupewa rushwa - nakuipokea kwa moyo mkunjufu - sio kitu cha ajabu - lakini hoja inarudi kwenye Rushwa yenyewe ni Nini?


Nchi nyingi za Kiafrika Zimeuzwa kwa Wageni tangu Kabla ya Ukoloni
kwa Mikataba Mibovu ambayo kwa nyuma mingi huambatana RUSHWA


Taarifa kwamba KIKWETE ALIPEWA RUSHWA YA SHOPPING, na Suti kama Tano hivi inazidi kumimina Chumvi kwenye vidonda vilivyojaa mioyoni mwa Watanzania! Watanzania wamekuwa na Kikwete kama rais wao kwa miaka kama Sita sasa na Ameonesha kwa Kiwango kikubwa sana KUSHINDWA kukabili Changamoto zinazolikabili.


KIKWETE AMESHINDWA kutoa suluhisho kwa Matatizo hata madogomadogo sana ambayo hata mtoto wa Sekondari akipewa mamlaka na madaraka ya kisheria na kikatiba aliyonayo Rais wa Tanzania angeweza kuyafanya!!!


Kiongozi aliyekaa madarakani kwa miaka 6 halafu mwaka wa Sita NDIPO ANAAHIDI kuwashughulikiwa waterndaji ndani ya serikali yake wanaokula Rushwa (wengi wao wakiwa ni wale aliowateua yeye mwenyewe); Hainishangazi hata kidogo kusikia AMEHONGWA NGUO!!!!!!



Viongozi wengi wanaouza nchi zao baada ya hapo hudharauliwa na
kuonekana kama "wavulana" machoni pa "wanunuzi"....
Madhara yake huwa ni mabaya zaidi kwa taifa zima




Kitendo hiki kilichofanyika karne hii ya 21 kinaumiza zaidi pale kinaponikumbusha Historia tuliyofundishwa na Wazungu! Historia hiyo tuliyofundishwa inasema Wasukuma wa Shinyanga wali "uza" Almasi za mwadui kwa kubadilishana na Pipi walizopewa na Wazungu!!


Historia hii pamoja na kuniumiza, nilijitahidi kutokuiamini kwa sababu iliandikwa na Wazungu, hivyo nikadhani labda ililenga tu kudhalilisha utu wa mtu mweusi --- SASA NAYAONA MWENYEWE!!!


Kwa mtu aliyeko Mwadau mwaka 1880, ninaweza kumuelewa kwa urahisi sana kupokea Pipi na kutoa Almasi kuliko mtu anayeishi mwaka 2011, Mwenye Digrii ya Chuo Kikuu, Rais wa Nchi, Anayemiliki Ndege ya kifahari ya Ofisi yake - Kuhongwa Suti NA MWARABU!!!


Pamoja na kwamba haya yanaumiza na kudhalilisha taifa, mimi hayaniumizi sana kwa sababu Tangu Kikwete hajachaguliwa kuwa Rais mwaka 2005 niliwaambia Watanzania KIKWETE HAFAI KUWA RAIS WA NCHI...!!! Imani yangu haijabadilika, na inazidi kupata Uthibitisho wake...


Pole Tanzania, Pole Afrika kwa yanayokusibu.... Namuomba Mungu akuwezeshe eeh Tanzania na wewe Mama Afrika kuzaa Watoto watakaokuwa Tofauti na Hawa ulionao sasa hivi!!!


N.B: Sijui kama Kikwete alihongwa kweli hizo nguo, na hivyo sijasema alihongwa. Hoja yangu imejikita katika "tuhuma" hiyo, na sio ukweli au uongo wake...

Monday, August 29, 2011

KIKWETE: IKULU INAPWAYA!


Juzi wakati nimewasili tu kutoka katika mizunguko yangu kusini mwa Afrika nilikutana na Gazeti moja likuwa na kichwa cha Habari kisemacho KIKWETE KIGEUGEU! Wakati nikiwa bado natafakari uzito wa maneno kusemewa kiongozi wa Nchi na yeye akayasoma na watu wanaomzunguka wakayasona na kumuonesha kwamba anasemwa hivyo wazi wazi, jana nikakutana na lingine lenye kichwa cha habari IKULU INAPWAYA!

Kunishtua na kunishangaza kwa maneno haya hakukutokana na uongo wake au upya/ugeni wake katika fikra zangu (kwa maana MIMI BINAFSI naamini kwamba ni ya Kweli kabisa). Mshituko wangu ulikuwa katika hatua ambayo Tanzania imefikia kwa sasa.

Tumeizoea Tanzania inayoongozwa na Rais mtendaji, ambaye anajitahidi kuonesha busara, ufahamu, ujuzi, dira na upeo wake yeye binafsi katika kushughulikia matatizo yanayoibuka na kulikabili taifa. Jitihada za marais hao tuliowazoea zilifanya watanzania wengi kuamini kuwa Matatizo waliyonayo yataisha kwa maana Rais wao yumo anayashughulikia.

Imani hii ya wananchi kwamba WANA RAIS IKULU ambaye anashughulikia matatizo na changamoto zinazolikabili taifa (hata kama hafanyi hivyo), ziliwafanya wananchi wengi kumshangaa, kumkemea na hata kumpinga wazi wazi mtu yeyote aliyekuwa akijitokeza na kutoa Kauli zinazoonesha kumsanifu, kumkejeli, kumdharau au kutokutambua jitihada zinazofanywa na Rais wa Nchi katika kushughulikia matatizo yao.

Miaka michache iliyopita (namaanisha KABLA YA KIKWETE hajaingia madarakani), kauli yoyote iliyokuwa inatolewa na mtu, taasisi au chombo cha habari KUMUHUSU RAIS WA NCHI ilikuwa inajadiliwa sana, kuchambuliwa na wakati mwingine kupingwa na kulaaniwa hadharani kwamba ni ya kichochezi, ni yenye kudharau mamlaka au kubeza jitihada za kiongozi.

KIKWETE analaumiwa kwa mambo mengi, sio tu kwa
Kutokuamua pale anapotakiwa Kuamua,
bali hata kwa maamuzi MABOVU.
ETI Chenge naye aliwahi kupewa Uwaziri na Kikwete!!!


HALI HAIKO HIVYO TENA!
Tangu ndugu yangu huyu ameingia madarakani kwa mbwembwe na kishindo, MAMBO YAMEBADILIKA SANA. Sidhani kama kuna Mtanzania yeyote mwenye akili timamu leo ambaye anaiheshimu Ikulu kwa heshima ile ya enzi za Mwalimu wa kwanza (acha mwalimu wa Pili) au basi hata enzi za Mwandishi wa Habari BM.

Moja ya Watanzania (sina hakika kama ni Mtanzania anyway) waliowahi kuwa na tuhuma nyingi sana za UFISADI NA UOZO wa kisiasa ni Rostam. KIKWETE ALISHINDWA KUSEMA AU KUFANYA LOLOTE DHIDI YAKE!

Kupwaya, katika matumizi ya kawaida, huwa ni ile hali ya kuingiza kitu kimoja katika kitu kingine na baadaye kubaini kwamba kile kilichoingizwa ni kidogo ukilinganisha na saizi ya kile kinachopokea! Kuna mifano mingi sana ambayo inaweza kutumika kuelezea upwayaji wa kitu fulani, lakini mfano rahisi zaidi ni ule wa mguu na kiatu! Pale WATU WANAPOSEMA KIATU KINAPWAYA, HAWAMAANISHI KWAMBA KIATU NI KIKUBWA BALI HUMAANISHA MGUU NI MDOGO!

IKULU INAPWAYA
Tangu kuingia kwa Kikwete katika Ikulu ya Tanzania na kutangazwa kuwa Rais wa Tanzania, kuna mambo mengi sana ambayo yamejitokeza yakimuhusisha yeye au watendaji walioteuliwa na yeye ambayo ukiyachunguza Hata kwa akili ndogo sana, utabaini kuwa kuna Pengo kubwa sana katika Ikulu ya Tanzania. Mambo mengi alyoyaamua, aliyoyafanya, ambayo hakuyaamua na ambayo hakuyafanya Kikwete, kwa ujumla wake yanaonesha kuwa kuna kitu kikubwa sana kinapingua Ikulu!

KIKWETE analaumiwa kwa tabia yake ya Kupenda kuzunguka
Duniani na kusifiwa na Viongozi wa Mataifa tajiri wakati hali ya kimaisha
ya Watanzania inaendelea kuwa mbaya
Anapokutana na Kusalimiana na WAZUNGU huonekana
kama alikuwa haamini kama kuna atakuja
kushikwa mkono na Mtu Mkubwa kama huyo!


Upungufu ambao unaambatana kwa kiasi kikubwa na HOFU ya kufanya maamuzi, kufanya maamuzi MABOVU, kutokuchukua hatua pale inapotakiwa, kuonesha kwa maneno na kwa matendo kwamba kuna Woga n.k. ni mambo ambayo yamewashawishi Watanzania wengi zaidi kuamini kuwa IKULU YETU INAPWAYA – TENA SANA!

Ndio maana katika Tanzania ya Leo, mtu kusema au kuandika waziwazi katika Gazeti kwamba RAIS WA NCHI NI KIGEUGEU, IKULU INAPWAYA n.k sio jambo linalohitaji kujadiliwa wala kukosolewa tena. Hata wale waliokuwa “waumini” wakubwa wa Serikali, ambao walikuwa tayari kuitetea Serikali ya nchi kwa gharama yoyote (ya maneno na majibizano), siku hizi WAMEJAWA AIBU na hawaoni kama kitu chochote cha kutetea katika Serikali na Ikulu yetu!

Mimi ningekuwa karibu na KIKWETE NINGEMSHAURI AJIUZULU awaachie nafasi watanzania Wamchague Rais, na akikataa kujiuzuru MIMI NINDIYE NINGEJIUZULU! Kuna watu wengine kufanya nao kazi wanaweza kukuchafulia CV na hata kukuharibia hadhi yako katika jamii na taifa kwa ujumla!

KIKWETE, NAKUSHAURI UJIUZURU TUCHAGUE RAIS!!!!

Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni.... Hakuna mtu ambaye
hukosea mambo yote, hata Kiwete kuna Mengine huyafanya kwa Usahihi....
Nakuachia Msomaji unitajie ni yapi anayoyfanya kwa usahihi

wasaalam....

Wednesday, August 24, 2011

GADAFFI: Kichwa Chake Chawekewa Fedha kama Osama!

Kufuatia kuangushwa na kusambaratishwa kwa Utawala wa Gadaffi na familia yake ambao umedumu kwa miaka 42, mfanyabiashara mmoja wa Libya amejitolea kutoa Zawadi ya Dola MILIONI MOJA NA NUSU (1,500,000.00 USD) kwenye "kichwa" cha Gadaffi

Mfanyabishara huyo amesema atatoa pesa hiyo kwa mtu yeyote atakaye muua au kumkamata hai Gadaffi...! Wakati huo huo wananchi wanaendelea kuji-sevia Bunduki na siraha nyingine mbalimbali nyingi zilizokuwa ndani ya majumba mengi na makubwa ya Gadaffi - LABDA - kwa matumizi yao ya baadaye au kwa ajili ya kumbukumbu!

Itakumbukwa kuwa rais wa Afghanistani pia (Mwalimu Mohammed Omar) naye aliwekewa kiwango cha fedha kadhaa juu ya kichwa chake - ambacho nadhani bado hakijatumika hadi sasa!

Picha hii hapa Chini Gadaffi akikumbatiana na mmoja wapo wa Marais wa Nchi za Kiafrika wakati wa utawala wake...

Gadaffi akikumbatiana na Mmoja wa marais wa nchi za kiafrika ambaye yeye, KWA BAHATI NZURI, bado ni rais nchini kwake

JAIRO Apokelewa kwa Shangwe Wizarani..!!!!!

Taarifa nilizozipata hivi karibuni nikiwa hapa Johannesburg, Afrika ya Kusini ni kwamba Davidi K. Jairo, katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na madini aliyesimamishwa kazi (kwa Kupewa Likizo YENYE MALIPO) kufuatia skendo za kutaka kuwahonga wabunge ili wapitishe bajeti ya Wizara hiyo (ambayo hata hivyo haikupitishwa na bunge) wiki kadhaa zilizopita AMERUDISHWA KAZINI!!!....


Taarifa zisizo Rasimi nilizozipata kwa kufuatilia mijadala mbalimbali (ikiwemo kutoka kutoka kwa mtu mmoja anayeonesha kuwa ni Mfanyakazi wa Wizara hiyo) zinasema kuwa Wafanyakazi wa Wizara hiyo walilipwa Posho kwa kuhudhurisha "hafla" ya Kumpokea Katibu huyo "KIPENZI" hapo wizarani....!!!


Hii Hapa ni nakala ya Barua aliyoisaini Jairo akiagiza Idara zilizo chini ya Wizara yake kuchangia ZAIDI YA SHILINGI BILIONI MOJA kwa ajili ya "kufanikisha" upitishwaji wa bajeti Dodoma! Chini ni Picha ya Jairo aliporejea Ofisini!

Hii ni nakala ya barua iliyosababisha Jairo kupewa
"LIKIZO YENYE MALIPO" kwa tuhuma za jaribio la
kuwahonga Wabunge


"MAMA ZETU" Wakimpokea "kipenzi chao" Jairo
kwa Shangwe nderemo na Vifijo Wakati aliporejea Ofisini..!!!
...Hii Ni Tanzania Zaidi ya Uijuavyo...!!!! TUMETHUBUTU, TUMEFANYA NA TUNASONGA MBELE!!!

Mdau mmoja alichangia hivi kuhusu huu Mjadala:

"JAIRO ...KWELI KAMANDA...WAKATI WA RICHMOND YEYE NDIYE ALIKUWA KATIBU WA WIZARA NA KAMATI YA MWAKYEMBE ALITAKA NA YEYE ACHUKULIWE HATUA...AKASAVAIVU.....H

UTETENZI WA CAG KUHUSU JAIRO
TUHUMA ZA JAIRO ILIKUWA NI KUKUSANYA BILIONI 1 KUTOKA KWA TASISI ZA SERIKALI ACCORDING TO BUNGE...LAKINI MCHUNGUZI WA CAG UMEONYESHA ALIKUSANYA MILIONI 500 NA SI BILIONI 1...KWA KUWA TUHUMA ZILIHUSU BILIONI 1 THEN JAIRO HANA HATIA....kwa kuwa wizara ina risiti ya matumizi ya hzo pesa

NIJUAVYO MIMI
hii sio issue ya CAG, kwa kuwa kazi ya CAG ni kuangalia kama matumizi ya pesa walifanyika kwa manufaa ya serikali,na sio kuangalia uhalali wa risiti...hata kama umefoji risiti unaweza ukawatoka CAG....hii ni issue ya TAKUKURU na POLISI kwa kuwa kuna mazigira na rushwa...na kufoji risiti

matumizi ya pesa
kati ya milioni 500 chenji ni milioni 123 ...huwenda zikatumika kumpongeza mzee kurudi kazini" Soma mchango huu wa Tumaini Thomas kwa
Kubonyeza Hapa...


Unaweza kufuatilia mjadala mmojawapo unaohusiana na kurudi kwa Jairo Kazini na kupokelewa kwa Shangwe kwa Kubonyeza Hapa...


Wasaalam... mussa