Tuesday, November 8, 2011

USHOGA: KIKWETE Umechangia Kutufikisha Hapa!

Kikwete akiwa na Waziri Mkuu
Mstaafu wa Uingereza ofisini kwake London.


Hivi karibuni Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron alitoa kauli moja ambayo sijui kama yeye mwenyewe alikuwa ameifikiria madhara yake kwa watu anaozungumza nao au la! Kwa Ufupi, alieleza kuwa Uingereza itaanza kuzuia misaada kwa nchi zinazopinga / zisizoruhusu uhuru wa Mashoga na Ushoga!


Hakujua Watu VIONGOZI (wa kiafrika) aliokuwa akizungumza nao ni Viongozi ambao wanaishi kwa kutegemea Misaada mingi kwa upande mmoja na kwa upande wa Pili wanaopenda kusifiwa na wananchi wao kila inapotokea fursa ya kuonesha kuwa wao ni mashujaa na majasiri - Cameron ALIKOSEA!


Kauli hiyo ilipokelewa "vibaya" na watu wengi Afrika, ikiwa ni pamoja na Watanzania! Serikali yetu haikupoteza muda kuirukia hiyo Fursa kwa ajili ya kujionesha kwa wananchi wake kuwa "haiburuzwi" kwa misaada, na ikatoa tamko kupinga kauli ya Cameron na ya kuonesha kuwa Serikali ya Tanzania iko tayari kukosa misaada ya Uingereza iwapo itakuwa na sharti la Ushoga (japo tulimpokea Mfalme wa Ushoga (Uingereza) kwenye Ikulu yetu jana kwa Mbwembwe na Sherehe kubwa)!!!!!!!!!!!
Kikwete hujisifia sana kukutana na watu maarufu,
 kupiga nao picha na Kuwaomba Misaada!


Usahaulifu wa Watanzania
Watanzania, pamoja na mambo mengine huwa wana sifa moja kubwa ya kusahau kwa haraka sana mambo na matukio muhimu yanayotokea kwenye jamii yao hata yale ambayo yanagusa sana maisha yao, na huwa wepesi wa kurukia mada / hoja mpya ambazo nazo huisha na kupotea haraka kwenye kumbukumbu na ufahamu wao.
Kikwete akipigwa-pigwa bega na Bush
baada ya kuahidiwa Msaada na Marekani!


Kikwete na Misaada
Sijui kama hapa Tanzania kuna Rais aliyewahi kufurahia kuomba-omba misaada, kufurahia kupewa misaada na kujivunia waziwazi na hadharani kupewa misaada na Wazungu KAMA KIKWETE! Nakumbuka Mkapa alikuwa mstari wa mbele katika kulipa madeni ili nchi ipewe misaada lakini sijui kama alifikia "rekodi" iliyowekwa na Kikwete.


Kwenye Kampeni za mwaka jana za Urais, Kikwete akihojiwa ITV, alitumia muda mwingi kujisifu kwa jinsi ambavyo amefanikiwa kuzunguka karibu dunia nzima - na mara zote watu walipokuwa wakipinga safari nyingi za Nje alikuwa AKIZIHALALISHA kwa KIWANGO CHA MISAADA alichokuwa anapewa / kuahidiwa na Wazungu!
Kikwete mara nyingi sana huonekana kwenye
Mikutano ya Kimataifa na wazungu, ambapo
hutumia nafasi hizo kuomba misaada
Kilicho NISIKITISHA SANA, KUNIUMIZA NA KUNISHANGAZA ni pale Kikwete - pasipo kuonesha anaelewa anachokisema - alipojisifu kwa jinsi alivyofikia hatua ya KUOMBA MISAADA KWA WATU BINAFSI (WAZUNGU) ili hao watu waje kuisaidia Nchi!!!!!!!!!!!!


Madhara ya Misaada!
Mimi ni mmoja wa Watanzania ambao wamekuwa msitari wa mbele kwa miaka mingi kupinga utegemezi wa misaada kwa taifa tajiri na lenye rasilimali nyingi kama Tanzania.


Siku moja nilimuuliza Mkurugenzi wa Benki ya Dunia iwapo misaada wanayotupatia inatusaidia na iwapo itatuwezesha kujitegemea alisema hiyo ni ndoto na tutaendelea kutegemea misaada kwa miaka mingi ija. Sehemu ya Taarifa hiyo inapatikana hapa: http://www.ippmedia.com/frontend/functions/print_article.php?l=13683
Sijui kama kuna rais yeyote mashuhuri ambaye Kikwete
hajawahi kukutana naye - na kuitumia hiyo nafasi KUOMBA MISAADA.
Hapa akiwa na Rais wa Ufaransa, Sarkozy
Sio tu kwa sababu misaada hudhalilisha "utu" wa taifa na watu wake, bali pia kwa sababu huwa ni mlango wa wale wanaotoa msaada kupenyesha ajenda zao katika taifa linalopokea misaada. Ukweli ni kwamba misaada ni zana ya kuzibana, kuzidhibiti na kuzinyanyasa nchi maskini kuliko inavyotumika kama chombo cha kuleta maendeleo.


Hii inajidhihirisha wazi kutokana na Masharti ambayo huambatanishwa na misaada katika nchi zote - ambapo masharti hutofautiana kutoka nchi moja hadi nyingine. 


Kwa mfano, wakati Nchi kama Marekani na Uingereza zinapotoa misaada kwa Tanzania na nchi nyingine za kiafrika husisitiza "Haki za Binadamu", "Demokrasia" n.k., Nchi hizo hizo zinapotoa misaada Pakistan, Afghanistan n.k. huwa haziweki mashari ya Demokrasia na Haki za Binadamu!!! Hii ni kwa sababu malengo yao huko yako tofauti na malengo yao kwa Tanzania na Afrika!


Uhusika wa Kikwete
Tabia ya Rais wetu kuwa mstari wa mbele katika kuzunguka duniani kuomba-omba misaada na kujisifu kwa jinsi anavyopewa misaada ndiyo imechangia kwa kiasi kikubwa leo tunaona kauli ya Cmaeron kuwa tishio.
Kikwete akisaini Mkataba wa "Msaada" kutoka Marekani


Kikwete angekuwa ametumia muda mwingi wa utawala wake kusimamia ukusanyaji, utumiaji na uendelezaji wa rasilimali za taifa hapa ndani ya nchi leo watanzania wasingeona kuwa kauli ya Cameron inalihusu taifa Letu!


Kilichotushitua wengi, na tukakimbilia kuisifu serikali kwa kauli yake ni mtazamo, akili na fikra zatu ambazo wote tumeaminishwa kuwa Misaada ni kitu muhimu na cha lazima sana kwetu, hivyo jambo lolote likisemwa kuhusiana na misaada lazima lituguse sana - JAPO HAIKUPASWA KUWA HIVYO!!!


Kitendo cha Kiongozi wa Nchi yetu kutokuweka msisitizo katika kuwawezesha Wananchi na Serikali yao kumiliki na kuendesha nyenzo kuu za Uchumi wa Taifa kama Sekta za Madini na Utalii na badala yake kukimbilia kuwaita Wazungu waje kuwekeza, kimeliacha taifa "UCHI" kwa kiasi kikubwa sana mbele ya Wazungu na Wageni wengine.
Kikwete huzunguka na Kukutana na watu wengi Maarufu
ambao huwakaribisha Nchini kama "Wawekezaji"...


Tabia ya kuwa na kiongozi anayezunguka dunia nzima kuomba misaada na kisha kuja kujisifu kwa raia zake pale anapopewa misaada ndicho mlango mkuu kwa taifa kuweza kuingizwa au kujiingizwa katika masharti magumu na mabaya ambayo wakati mwingine yanalidhalilisha Taifa na Raia wake!



Mapendekezo yangu
Wakati taasisi za Kidini, vyama vya siasa na wananchi tukiendelea kumimina sifa zetu kwa "Membe" kwa kauli yake ya kupinga Sharti la Ushoga, ni lazima tuangalie na kubaini kuwa  mlango huo wa Masharti ya Ushoga Umetokana na nini.


Mlango huu tumeufungua wenyewe kama taifa, tukiongozwa na "viongozi" wetu wa sasa na waliopita. Tumeufungua kwa kuamua kama taifa kuacha kuwajibika kwa namna ipasavyo katika kujipanga kitaifa kutumia na kunufaika na rasilimali zetu wenyewe, badala yake tumeamua kwa makusudi kama taifa KUWAONA WAZUNGU KAMA MIUNGU ambayo haiepukiki ili tuweze kuendelea kama taifa.


Kasumba ya kupenda na kusifia MISAADA YA WAZUNGU imetufanya tufikie mahali tuone kama vile hatuwezi kuishi bila kufanya ziara za Ulaya, Hatuwezi kutumia na kunufaika na rasilimali zetu bila kuwauliza na kusaidiwa na Wazungu n.k.


Hili la Ushoga ni moja, tukiendelea na tabia hii ya kuwa na SERIKALI LEGELEGE katika kushughulikia maendeleo ya kitaifa, muda si mwingi tutapewa masharti magumu zaidi ya Ushoga, na kwa UPUMBAVU WETU tutalazimika kuyakubali Ili tuendelee kupokea misaada!


Tuchukue Hatua
Moja ya mambo ya msingi ambayo tunapaswa kuyafanya kama taifa, ni kurudi kwenye msingi alioanza kutujengea baba wa taifa wa Kujitegemea kama taifa. Hii kasumba ya kuwaabudu wazungu na kujiona kama vile sisi hatuwezi kitu pasipo Wazungu ndiyo imetufikisha hapa na Itatufikisha pabaya zaidi!
......


Kama taifa, tunapaswa kujipanga na kutafuta njia zinazoweza kulisaidia taifa na raia wake kutumia na kunufaika na rasilimali zao badala ya kuendelea kujisifia LUNDO LA WAZUNGU ambao huwa tunawapamba kwa majina ya wabia na wawekezaji - wakati wengi wao ni wanyonyaji tu!


Hitimisho langu kwa Leo
Mimi naamini hata kwa misaada ambayo tumeshapewa, tunaendelea kupewa na tunaendelea kuipokea, TAYARI TUMESHAKUBALI MASHARTI MENGI KULIKO USHOGA, na tunajisifia kwenye hotuba zetu na kampeni zetu za Uchaguzi!!!


Kasumba hii ya kuwa na Viongozi VIPOFU NA MASKINI WA FIKRA, wasioamini kwamba Tanzania na watanzania wanaweza kuendelea pasipo misaada ya Wazungu imeshatuponza sana na itaendelea kutuponza sana.


Kauli za Kupinga masharti ya Ushoga kwenye Misaada
hazitatusaidia iwapo hatutachukua hatua za
Kuachana na Utegemezi wa Misaada na Badala yake
Kujisifia kutembelewa / kukutana na Marais Maarufu Duniani!
Tusipobadilika kama taifa, kauli kali za kujifanya tuna uhuru hazitalisaidia hili taifa iwapo tutaedelea kuwa na viongozi wasio amini kuwa Tanzania inaweza kuendelea kwa jitihada zake pasipo misaada ya Wazungu!!!

3 comments:

  1. sisi watanzania ni watu wa ajabu,ndo maana kila siku tutakuwa watu wa nyuma tu kama {koti}wakati huu wakati mallikia wao akiwa nchini ndo kipindi tungeonyesha umuhimu wa watanzania ata kuingia ikula kwa nguvu na mabango yetu tukimpiga malkia na vitendo vyao vya ushogo wakafifanyie kwao hatuwaitaji TANZANIA,BORA WATANZANIA WOTE KUFA NA NYAJAA KULIKO KUZALILISHWA.

    ReplyDelete
  2. labda ni muhimu kufahamu pia kuwa huyo "Malkia" unayemzungumzia AMEALIKWA NA KIKWETE, hakuomba yeye kuja, ALIOMBWA NA KIKWETE AJE TANZANIA....!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete