Tuesday, October 25, 2011

PICHA ZA GADDAFI: Uhai na Kifo Chake!

Picha Zote ni kwa hisani ya Mashirika ya Habari ya Kimataifa na Mtandao wa Intaneti.
Col. Muammar Al Qaddafi


Hapa akiwa Addis Ababa akikumbatiwa na Mmojawapo wa Marais wa Afrika

Mwishoni mwa Miaka ya '00 "aligeuka na kutubu" na kuamua kuwa "mtoto mzuri" machoni pa Wazungu

Hadi Alikuwa na Album ya Picha za Condoleeza Rice tu Ikulu...!!!!

Vuguvugu la Nchi za Kiarabu lilipoingia Libya, Taifa liligawanyika - WACHACHE wakimuunga Mkono WENGI wakimpinga


Kwa Sababu Vita kama hizi huwa sio za Siraha tu, bali na Vita ya "publicity", hadi Lugha za Kigeni zilitumika katika kuifahamisha Dunia kwamba Gadaffi ana wanaomuunga mkono 



  


Vita ilipochanganya kwa miezi kadhaa na mashambulizi ya NATO KUZIDI, mwezi wa Ogasti ilivumishwa kwamba Gadaffi ameuawa kwenye shambulio la NATO, na Picha hii feki ilisambazwa kwenye mtandao kwamba ni ya maiti yake. 

Ukweli ni kwamba picha hii SIO YA GADAFFI, ni ya kijana mmoja aliyeuawa na Wamarekani siku waliposhambulia nyumbani kwa Osama na kumuua, huko Pakistan.
Picha Ilibadilishwa Hivi
Hatimaye, mwezi Oktoba, Alhamis tarehe 20, Qaddafi akiwa ni walinzi wake walishambuliwa na ndege za NATO ambazo ziliwaua walinzi wake na yeye akafanikiwa kuponyoka na kujificha kwenye hii "karavati" kabla hajakamatwa na Askari wa NTC akiwa hai (na majeraha kidogo sana)
 Muda mfupi baadaye, taarifa na picha zilionesha kwamba amekufa - katika mazingira ya kutatanisha. Inasadikiwa kuwa aliuawa na walewale waliomkamata - jambo ambalo ni kinyume cha sheria za kivita. Hata hivyo, uwezekano wa yeye kuuliwa mara moja ulikuwa ni mkubwa sana kwa sababu alikamatwa na Vikosi vilivyotokea mjini Misrata. Misrata ni moja ya miji iliyowahi kushuhudia mauaji makubwa kabisa ya raia na wakazi chini ya Utawala wa Miaka 42 ya Qaddafi, na hususan, baada ya vuguvugu la mapinduzi kuanza. Hivyo ni wazi kuwa "alianguka" mikononi mwa mahasimu wake wakubwa. 

Maiti yake ilisafirishwa kutoka Sirte alikokamatwa na kuuliwa hadi Mjini Misrata, vilikotokea vikosi vilivyo mkamata. Huko Misrata, maiti iliwekwa kwenye Kontena la Barafu la Kutunzia Nyama ili kusaida isiharibike na likaachwa wazi kwa ajili ya maonesho ya watu kupiga picha na kushangilia....

Baadaye ilibainika kuwa kontena hilo lilikuwa halifanyi kazi ipasavyo (labda kutokana na kuachwa wazi) na hadi leo Asubuhi, Jumanne tarehe 25, mwili wa Qaddafi na mwanawe aliyeuawa siku hiyo hiyo Martassem ilikuwa imeharibika na inatoa harufu kali sana. Serikali iliamuru azikwe lakini mvutano ulikuwa ni mahali pa kuzikwa.



 Kanali Mouammar All Qaddafi, Shujaa kwa Baadhi na Muovu kwa Wengine - Utawala wake wa Miaka 42 na ndoto zake zote kuihusu Libya na Afrika Zimepotea ndani ya Miezi SITA tu!

"Innalillah wa yna Lillayih Rajiun"

22 comments: