Wednesday, September 14, 2011

UNAFIKI WA CCM: Rostamu: Shetani-Malaika KWA WAKATI MMOJA????

Jina la Rostam ni jina maarufu sana masikioni mwa Mamilioni ya Watanzania - japo wengi wao ni kwa Ubaya, Chuki, hasira, Uchungu na....
Alijiuzuru Kutokana na Kuchoshwa na SIASA UCHWARA
ZA CCM.... LEO ANAWAOMBA KURA WANANCHI
WAKICHAGUE CHAMA CHENYE SIASA UCHWARA!!!!
Hivi karibuni, Muhasibu huyo mstaafu wa CCM Taifa, Kada wa Chama, Mjumbe wa Halmashauri ya CCM, NEC nakadhalika alikuwa Gumzo kubwa Ndani ya Chama hicho, kwenye vyombo vya habari na nchini kwa Ujumla kwamba YEYE ROSTAMU pamoja na wenzake Wawili NDIYO MAGAMBA ambayo Mwenyekiti wa Chama KIKWETE alikuwa anawaongelea kwenye maadhimisho ya Miaka 34 ya CCM mwezi Februari.


Baada ya hapo, Chama kilivunja Sekretariat na kuunda mpya ambayo ilianza kazi kwa Mbwembwe sana, kubwa ikiwa ni kutishia kuwavua "magamba" wa Chama hicho iwapo hawatajivua wenyewe ndani ya Siku 90! Baadaye ilikuja kufahamika kwamba ULIKUWA NI UONGO WA CCM kama kawaida ya Chama hicho! Siku 90 zilipita na hakuna kilichofanyika!


Siku kadhaa baadaye, Rostam Azizi, Mbunge wa Jimbo la Igunga (CCM) na kada mkuwa wa CCM aliamua kujiuzuru Ubunge na Siasa kwa sababu kubwa aliyoitaja kuwa ni SIASA UCHWARA za ndani ya CCM..!!! Aliposema CCM ina Siasa Uchwara, naamini alikuwa anamaanisha Kabisa kwamba KIKWETE, Mwenyekiti wa CCM ANA SIASA UCHWARA kwa maana Yeye ndiye Mwenyekiti na Kiongozi wa Chama hicho Chenye Siasa Uchwara!
Watu wanaofahamika wazi kuwa ni Mafisadi, Wanafiki,
Wasaliti wa Taifa hukemewa tu iwapo hakuna kampeni,
kampeni zikija huonekana ni wa Muhimu kwa Ushindi
na Hutumiwa "kurubuni" wapiga kura...
Mchakato wa kumpata Mrithi wa Rostam ulipoanza, nilishangaa kupata taarifa kuwa CCM Imepanga Kumtumia Rostam Azizi kufanya Kampeni ya Chama hicho Igunga!!!... Nilidhani utani kwa sababu ni UPUMBAVU ambao hata mtoto mdogo asingeweza kufikiria kwamba Chama "kikongwe" cha Siasa kama hicho kinaweza kuwa na maamuzi ya "kijinga" namna hiyo...


Rostam, ambaye Amesimangwa sana, amesemwa sana - kwa mafumbo na kwa wazi wazi na CCM... Rostam, aliyejiuzuru Ubunge kutokana na Siasa Uchwara za CCM, Leo ndiye anaongoza Kampeni za Kumpata Mrithi wake Kwa Idhini ya Chama hicho hicho chenye Siasa Uchwara?????


Kama Wananchi wakimsikiliza Rostam na Kumchagua Mbunge kutoka Chama Chenye Siasa Uchwara, nitajua Tatizo la Uchwara SIO LA CCM BALI LA WANANCHI..!!!


WANANCHI WAKICHAGUA MBUNGE KUTOKA KWENYE CHAMA CHENYE SIASA UCHWARA, NITAJUA ZAIDI KWAMBA TATIZO KUBWA LA HII NCHI SIO UCHWARA WA SIASA ZA CCM BALI UCHWARA WA AKILI ZA WATANZANIA!!!!

3 comments:

  1. huu ndio undumakuwili wa CCM,Siku zote wamekuwa hivyo,wanatenda kinyume na wanavyoongea,

    ReplyDelete
  2. pamoja ndugu yangu lakini ingefaa haya yakawafikia wana igunga.

    ReplyDelete