Thursday, September 22, 2011

TGNP na USHOGA/USENGE: Shutuma Zazidi Kuongezeka!



Stanslaus Nyembea
Dar es salaam
                                                                                                                                     September 22, 2011
MTANDAO WA JINSIA TANZANIA-TGN
P.O.BOX P.o.Box 8921
Dar es Salaam
Tel: +255 22 2443450
TO WHOM IT MAY CONCERN
YAH: MAONI BINAFSI JUU YA HALI YA USHOGA NA TAMASHA LA JINSIA
Mimi ni miongoni mwa wanaharakati wa masuala ya haki za binadamu, maliasili na mazingira. Nimekuwa nikipigania haki za kimsingi za kibinadamu kwa nadharia na vitendo. Ushiriki wangu umesaidia kupambana na ukiukwaji wa haki za binadamu kwa namna moja au nyingine katika nchi yetu na nchi jirani.
Nitumie fursa hii kuipongeza kwa dhati kabisa Tanzania Gender Networking  Program (TGNP) kwa mchango wake wa kuleta mabadiliko chanya katika jamii ya kitanzania. Mchango wa TGNP ni mkubwa na wanaharakati wa haki za binadamu, rasilimali na Mazingira kwa ujumla wanautambua na kuuthamini.
Baada ya pongezi hizi, napenda kutoa maoni yangu juu ya Tamasha la Jinsia liloandaliwa na TGNP kuanzia tarehe 13-16 katika viwanja vya TGNP.
Ni kweli kuwa kuna mambo mazuri mengi yalifanyika wakati wa Tamasha hili, ikiwemo jamii za pembezoni kutoa na kupaza sauti zao kuhusu masuala mbalimbali nyeti yanayozifanya jamii hizi kukosa au kunyimwa haki zao za  kimsingi za kibinadamu.
Pamoja na hayo mazuri, kwa maoni na mtizamo wangu, mazuri hayo yalifutwa kabisa na msimamo na upigiaji chapuo  wa TGNP kuhusu masuala ya USHOGA katika jamii ya kitanzania. Binafsi sikatai uwepo wa USHOGA/USENGE katika jamii ya kitanzania. Sina mtizamo wa kihafidhina wala wa kuwatenga watu hawa, lahasha. Tatizo langu ni kupigia chapuo kwa TGNP suala hili la USHOGA/USENGE.
Hoja yangu ya kupingana na TGNP kuhusu mtizamo wenu ni jinsi mlivyolichukulia na kulienzi suala hili. Nashindwa kupata dhamira nyingine zaidi ya kuwa TGNP mna malengo kadhaa na suala hili. Nashawishika kuamini kuwa mnapigania kuleta mabadiliko hasi kwa jamii yetu, yaani jamii ya kitanzania ilione suala hili kuwa la kawaida, hivyo watoto wetu wajihusishe na USHOGA/USENGE.
Pengine, utetezi wenu kuwa mnataka jamii ijue kuwa tatizo hili lipo na ichukue hatua. Lakini hoja hii haina mashiko wala miguu.
Utetezi wenu pia kuwa watu hawa, MASHOGA/WASENGE wameingia katika matendo haya machafu kwa sababu za kiuchumi na kibiojia nayo hayana maantiki hata kidogo.
Je, mbona masikini wa Tanzania wapo wengi tu! Na wao mnataka waingia katika USHOGA/USENGE? Je ukishakuwa SHOGA/MSENGE ndiyo matatizo ya kibiolojia na kiuchumi yanaisha? Nini mnataka watoto wetu wafanye zaidi ya kuona USHOGA ndiyo suluhisho la umasikini?
Je kama watoto wenu wangekuwa mashoga/wasenge mngewaleta kwenye tamasha hili?
Jibu rahisi ni kuwa TGNP mnapata fedha za kuwa na miradi hii toka kwa mashoga/wasenge wa kimataifa wanaotaka kufanya jamii nzima iwe kama wao. Ni tamaa ya fedha tu ndiyo inayowafanya mpigie debe suala la ushoga/ushoga nchini mwetu na si vinginevyo. Kuna tofauti gani kati ya RUSHWA/UFISADI mnaoukataa katika serikali yetu na kutumia fedha chafu za watetea USHOGA/USENGE. Fedha yao ni chafu, hata ikitumika kuutokommeza USHOGA bado itakuwa chafu tu.
Je, unaweza kutumia fedha ya mtetea USHOGA/USENGE kuwafanya mashoga waache tabia hii? Mbona haiwezekani! Lengo ni kuwatetea tu waendelee na tabia hii chafu na si vinginevyo.
Vile vile naona TGNP kupoteza staha na heshima iliyojijengea katika jamii yetu ya Tanzania kwa muda mrefu. TGNP kwa kujiingiza kwenye suala hili ni kupoteza dira na mwelekeo sahihi. Siwahukumu ila ndiyo ukweli mwenyewe. Mnataka tuwe na taifa la aina gani? La mashoga/wasenge? Ukuaji wa taifa utakuwaje ikiwa watu wote watakuwa kama dhamira ya wasenge ilivyo?
Uungwana huanzia nyumbani. Ikiwa matendo na sera zenu zitakosa staha kwa watanzania kazi yenu itakuwa ni mfu na isiyo na tija. Uungwaji mkono wenu wa kwaida utapotea sana.
Nawasihi mtafakari upya mwelekeo wenu ili heshima na staha yenu irudi kwa watanzania. Kuteleza siyo kuanguka, chukueni hatua hamjachelewa. Chukueni maamuzi magumu ya kukataa fedha za watetea USHOGA/USENGE. Zipo nyingi tu na ndizo zilizowaingiza katika mtego huu mchafu.
Stanslaus Nyembea

2 comments: