Wednesday, August 24, 2011

GADAFFI: Kichwa Chake Chawekewa Fedha kama Osama!

Kufuatia kuangushwa na kusambaratishwa kwa Utawala wa Gadaffi na familia yake ambao umedumu kwa miaka 42, mfanyabiashara mmoja wa Libya amejitolea kutoa Zawadi ya Dola MILIONI MOJA NA NUSU (1,500,000.00 USD) kwenye "kichwa" cha Gadaffi

Mfanyabishara huyo amesema atatoa pesa hiyo kwa mtu yeyote atakaye muua au kumkamata hai Gadaffi...! Wakati huo huo wananchi wanaendelea kuji-sevia Bunduki na siraha nyingine mbalimbali nyingi zilizokuwa ndani ya majumba mengi na makubwa ya Gadaffi - LABDA - kwa matumizi yao ya baadaye au kwa ajili ya kumbukumbu!

Itakumbukwa kuwa rais wa Afghanistani pia (Mwalimu Mohammed Omar) naye aliwekewa kiwango cha fedha kadhaa juu ya kichwa chake - ambacho nadhani bado hakijatumika hadi sasa!

Picha hii hapa Chini Gadaffi akikumbatiana na mmoja wapo wa Marais wa Nchi za Kiafrika wakati wa utawala wake...

Gadaffi akikumbatiana na Mmoja wa marais wa nchi za kiafrika ambaye yeye, KWA BAHATI NZURI, bado ni rais nchini kwake

No comments:

Post a Comment