Monday, August 15, 2011

MAFUTA Kupanda Bei Tena Wiki 2 Zijazo!



Niliposoma hii taarifa hapa chini nilijiuliza maswali mengi sana ikiwa ni pamoja na: 


  • Ni Nani anayewajibika kudhibiti kupanda na kushuka kwa thamani ya Shilingi?
  • Ile Stoke ya Mafuta iliyodaiwa na Ngeleja kwamba inaweza kudumu kwa Siku 60 imeisha lini, mbona Mafuta yamepanda ghafla?
  • Ina maana Serikali iliposema itapunguza bei ya Mafuta kwa mwaka huu wa fedha ILIKUWA INADANGANYA ili kuwezesha kupitishwa kwa bajeti yake? 
  • Hivi wanaofanya haya MAAMUZI YA KIPUMBAVU wanadhani kwamba Taifa hili limejawa na Watu wapumbavu tu?....
Maelezo na Visingizio vilivyotolewa na EWURA jana vinaonesha Wazi kuwa WIKI MBILI ZIJAZO Mafuta yatapanda bei tena, kwa sababu hakuna dalili zozote zinazoonesha kwamba Shilingi itapanda thamani wala kwamba mafuta yatashuka bei kwenye soko la dunia!

Taifa hili limebaki kama yatima!

Meneja Biashara wa Mamlaka ya Udhibiti wa

 Huduma za Nishati (EWURA)
Mhandisi Godwin Samweli 


SERIKALI YASEMA NI SABABU YA KUANGUKA KWA SHILINGI NA BEI KATIKA SOKO LA DUNIA 
Fidelis Butahe
SIKU kumi na moja baada ya kutangaza kushusha bei ya mafuta nchini, hatua ambayo ilisababisha mgogoro mkubwa uliotishia uchumi wa nchi, jana Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imeongeza tena bei ya nishati hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Meneja Biashara wa Ewura, Godwin Samwel alisema petroli imepanda kwa Sh 100.34 sawa na asilimia 5.51, dizeli kwa Sh 120.47 sawa na asilimia 6.30 na mafuta ya taa kwa Sh 100.87 sawa na asilimia 5.30 na kwamba bei hizo zitaanza kutumika kuanzia leo.

Alisema bei hizo mpya zimetokana na kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na kuendelea kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania, ikilinganishwa na Dola ya Marekani.

Hatua hiyo ya Ewura imekuja siku moja baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka 2011/12.

Agosti 3, Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu alitangaza bei elekezi iliyoshusha bei ya nishati hiyo ili kumpunguzia makali mwananchi wa kawaida na kusema kwamba petroli ilishuka kwa Sh202.37 kwa lita sawa na asimilia 9.17, dizeli Sh173.49 sawa na asilimia 8.32 na mafuta ya taa kwa Sh 181.37, sawa na asilimia 8.70.....
Soma hii habari ya Mwananchi kwa ukamilifu kupitia http://www.mwananchi.co.tz/component/content/article/37-tanzania-top-news-story/14505-serikali-yapandisha-tena-bei-ya-mafuta.html

No comments:

Post a Comment