Monday, May 7, 2012

MAWAZIRI Wapya: Wataleta Mabadiliko Chini ya Kikwete Huyu Huyu?

Wiki iliyopita Rais Kikwete litangaza baraza jipya la Mawaziri, likiwa na sura nyingi za zamani. Maamuzi haya yalitokana na shinikizo kubwa kutoka kwa wananchi wengi na wabunge wa vyama mbalimbali wakiwemo wa chama anachokiongoza yeye mwenyewe!
 
Janeth Mbene, Naibu "mpya" wa Waziri wa Fedha
Wakati mabadiliko haya yanaweza kumaanisha kuwa yanatakiwa mabadiliko, swali linabaki, uongozi wa nchi hii unaweza kubadilika kwa kubadilishwa kwa baraza la mawaziri kwa "lazima"  wakati Rais bado ni Kikwete huyo huyo?

Kuchelewa kwa Kikwete kufanya maamuzi ambayo ni wazi kuwa yalitakiwa kufanyika zamani, na kitendo cha yeye kutoyafanya mpaka alipotishiwa na wabunge hadi wa chama chake mwenyewe kuwa wangeiangusha serikali yake nzima iwapo asingefanya maamuzi inaacha maswali kadhaa ya msingi. Baadhi ya maswali ni pamoja na haya:

KWANZA: Je, Rais mwenyewe anaamini kwamba mabadiliko aliyoyafanya yalikuwa ni ya lazima kufanyika au ameyafanya ili kuwaridhisha waliokuwa wanayataka - japo alijitahidi siku nyingi kuwapinga mpaka walipomshinda nguvu!

PILI: Je, Mawaziri hawa wapya wataweza kuboresha uharibifu mkubwa ambao umeshuhudiwa katika serikali na nchi hii tangu Kikwete alipoingia madarakani - wakati yeye akiwa bado yuko Madarakani?.. Pamoja na mengine mengi.

Wakati tunaendelea kusubiri kuona kama mawaziri hawa wapya wataweza kuleta mabadiliko tunayoyataka katika taifa, ni muhimu watanzania tukaendelea kujiuliza - nchi hii itakuwa ni ya kufanyiwa majaribio ya viongozi mpaka lini? Ni lini ambapo tutakuja kuweka viongozi wenye sifa na uwezo madarakani ambao hawatupotezewa miaka mingi ya kusubiri kuwapa muda wafanye wanayoyafanya mpaka tunapokuja kubaini madudu na uozo waliokuwa wanaufunika?..
 
Wakati tukiendelea kusubiri kuona iwapo hawa watakuwa tofauti na waliowatangulia, nashauri tuutumie huu muda kujiandaa kwa kuwatambua watu wanaofaa kuliongoza hili taifa tangu sasa na tuwachague hao katika uchaguzi mkuu ujao - tusiendelee kuliweka taifa letu mikononi mwa watu "wanaojaribu" kuongoza tena, tuwape watakaoweza kuifanya hiyo kazi. Orodha ya Wizara, Mawaziri na Manaibu wao hii hapa chini!
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI


MAWAZIRI

 1. OFISI YA RAIS

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)

Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)

Ndugu George Mkuchika, Mb.,

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)

Ndugu Celina Kombani, Mb.,

2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)

Ndugu Samia H. Suluhu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)

Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,

3. OFISI YA WAZIRI MKUU

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)

Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)

Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,

 4. WIZARA

 Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,

 Waziri wa Ujenzi

Dr. John P. Magufuli, Mb.,

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii

Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,

 Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,

Waziri wa Katiba na Sheria

Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,

Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

Dr. David M. David, Mb.,

Waziri wa Kazi na Ajira

Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia

Prof. Makame M. Mbarawa, Mb.,

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb.,

Waziri wa Maji

Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,

Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum

Prof. Mark Mwandosya, Mb.,

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika

Eng. Christopher Chiza, Mb.,

Waziri wa Uchukuzi

Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,

 Waziri wa Maliasili na Utalii

Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,

Waziri wa Viwanda na Biashara

Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,

Waziri wa Fedha

Dr. William Mgimwa, Mb.,

Waziri wa Nishati na Madini

Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,

 5. NAIBU MAWAZIRI

  
OFISI YA RAIS

HAKUNA NAIBU WAZIRI

6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS

 Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais

Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,

7. OFISI YA WAZIRI MKUU

 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,

  
8. WIZARA MBALIMBALI

 Naibu Waziri wa Kazi na Ajira

Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika

Ndugu Adam Malima, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara

Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi

Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,

Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,

Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii

Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,

Naibu Waziri wa Ujenzi

Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,

Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,

Naibu Waziri wa Nishati na Madini

Ndugu George Simbachawene, Mb.,

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia

Ndugu January Makamba, Mb.,

Naibu Waziri wa Uchukuzi

Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,

Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

Ndugu Amos Makala, Mb.,

Naibu Waziri wa Maji

Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,

Naibu Waziri Nishati na Madini

Ndugu Stephen Maselle, Mb.,

 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria

Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,

 Naibu Waziri wa Fedha

Ndugu Janet Mbene, Mb.,

Naibu Waziri wa Fedha

Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu.

Dar es Salaam.

1 comment:

  1. What you havе written in "MAWAZIRI Wapya: Wataleta Mabadiliko Chini ya Kikwete Huyu Huyu?" is definitely not totаlly onlу grеat
    but аctually mοԁel of impоrtаnt.
    I know a number of people don't really keep in mind these products. But once you offer a similar experience to me and are sorted out losing weight or dependency or from associated with the the things you truly can thinking about I usually tend to appreciate what I read as it is really the actual easiest way to gain in knowledge with out actually doing the things. On this reason I enjoy finding out different peoples aspects of views and experience.

    Have a look at my weblog: 5htp.org
    My site: 5htp.org

    ReplyDelete